Google wametoa ujumbe wa kutaka watumiaji wa kivinjari cha Google Chrome kusasisha haraka iwezekanavyo – ikiwalenga zaidi watumiaji wa kompyuta.
Google wamegundua toleo lao lililopita linakosa flani kwenye utengenezaji, kosa ambalo linafanya iwe rahisi sana kwa wadukuzi wa kimtandao kudukua kompyuta ya mtumiaji.
Kwa wengi sasisho (update) hii itakuwa imerushwa moja kwa moja, ila kwa uhakika nenda na bofya eneo la ‘Help’ kwenye mipangilio ya kivinjari cha Chrome, kisha bofya ‘About Google Chrome’, hakikisha unatumia toleo la sasa – ambalo ni toleo 72.0.3626.121..
Kama utakuwa toleo la namba za chini ya hizi basi hakikisha unasasisha kwenda toleo jipya haraka iwezekanavyo.