Kivinjari cha Google Chrome ndio kivinjari kinachoongoza kutumiwa na watu duniani na hata upatikanaji wake ni kariabia kwa kila kifaa.
Kwa sasa makampuni mengi yanafanya juu jinni katika kuhakikisha kuwa wanapata sulihisho la kufanya ku’log in kuwa rahisi
Unakumbuka tualindika kuhusu Apple, Google Na Microsoft kuja na njia ya ku’log in vila kutumia nywila (password)? Soma zaidi >>HAPA<<
Kwa sasa Googe kupitia Chrome –kwenye kompyuta—inakuja na uwezo wa kuwezesha mtu kuweza kuingia kwenye kurasa zake za Google kwa kutumia skana ya alama za vidole katika kompyuta (laptop) yake.
Kumbuka kuna kompyuta mpakato (laptop) nyingi ambazo zina sehemu ya kuweka alama ya kidole (fingerprint) kama sehemu yake ya nywila/neon siri (password).
Kinachofanyika hapa ili kuwezesha hili ni lazima uwe na kompyuta yenye skana hiyo na pia uwe unatumia kivinjari cha chrome na kingine kikubwa ni kwamba inabdi uwe unatembelea kurasa za google kama vile Gmail, YouTube, Google Drive N.k
Hii itakua ni kwa watumiaji wote wa Windows na hata wale wa Mac, wote watapata huduma hiyo kupitia toleo jipya la Chrome linalojulikana…
…Kama Chrome v106 ambayo itakuja na huduma hiyo ya uthibitishaji wa bayometriki (Biometric) katika huduma mbalimbali za Google.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment, Je Hii Umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.