Ukiwa unatumia simu janja basi barua pepe ni ufunguo wa kuwa na uwezo wa kupakua programu tumishi mbalimbali kutoka sokoni. Kwenye Android ni lazima uwe na akaunti ya Gmail na kwa lugha rahisi tuu programu tumishi husika itakuwezesha kuandika/kusoma jumbe ulizotumiwa kirahisi kabisa.
Mpaka leo kuwa simu janja ambazo zina memori na RAM ndogo jambo ambalo linafanya simu kuzidiwa uwezo na ufanisi wake wa ufanyaji kazi kuwa mdogo kiasi kwamba mtu anapata kadhia kutumia rununu. Jambo hili ndio linasababisha makampuni mengi kutengeneza programu tumishi ambazo si kubwa hivyo kufanya simu kutekeleza majukumu yake vizuri tuu.
Google wameendelea kuja na programu tumishi mbadala mahususi kwa zile rununu zenye memori (diski uhifadhi na RAM) ambapo hivi sasa Gmail Go inapatikana kwenye Playstore. Kimsingi Gmail Go imetengenezwa ili kutoathiri ufanyaji kazi wa simu zenye uwezo mdogo. Mbali na hilo toleo la “Go” hakuna kitufe cha Google Meet na muonekano wake ni wa kawaida ila unafanana na programu tumishi kuu.
Kama unatumia simu janja ambayo ni Android na ina memori ndogo au hata kama rununu ina uwezo wa juu lakini hutaki memori ijae haraka basi ni vyema ukapakua Google Go, Facebook Lite, Messenger Lite, Twitter Lite na sasa Gmail Go kwa ajili ya matumizi ambayo hayataathiri ufanisi wa kifaa husika.
Vyanzo: GSMArena, Firstpost
No Comment! Be the first one.