Je aliwezaje? Fahamu gari la Steve Jobs halikuwahi kuwekwa namba za usajili/yaani plate number. Steve Jobs alikuwa anapendelea kutumia gari aina ya Mercedes ikiwa haina namba za usajili.
Steve Jobs alikuwa mbunifu na mkurugenzi wa kampuni ya Apple aliyefariki mwaka 2011.
Soma pia
Kwa muda mrefu, miaka na miaka watu wengi walishangaa kila Steve Jobs akionekana katika shughuli zake za kikazi au binafsi katika mitaa ya Silicon Valley gari lake lilikuwa vile vile – bila kuwa na namba za usajili.
Je aliwezaje kisheria?
Steve Jobs alifahamu sheria ya jimbo la California iliyohitaji gari jipya kuweza kutumika hadi miezi sita tuu bila ulazima wa kuwa na namba ya usajili. Kwa kifupi sheria ilikuwa inampa mmiliki wa gari jipya hadi miezi sita kuweza kukamilisha utaratibu wa kupata na kuweka namba ya usajili kwenye gari.
Steve Jobs alichofanya ni kuingia mkataba na kampuni ya kukodisha na kuuza magari ambayo ikawa ina mpatia gari jipya la aina ile ile – Mercedes SL55 AMG kila baada ya miezi sita. Kwa kifupi kila miezi 6 Steve Jobs alikuwa anapata gari jipya, na hivyo kisheria moja kwa moja alikuwa na haki ya kulitumia hadi miezi 6 bila kuweka namba ya usajili.
No Comment! Be the first one.