Facebook imekuwa ikiongeza vitu kwenye app ya kuchat ya messenger ili kuzidi kuwavutia watumiaji ili iweze kupakuliwa (download) na wengi na Facebook kuzidi kujiongezea kipato kutokana na kupakuliwa kwa application hiyo.
Sasa kuweza kucheza gemu ya mpira kwenye Facebook Messenger.
Kutokana na kuendelea kwa kombe la Euro 2016 facebook wameamua kuifanyia maboresho app yake ya FB messenger kwa kuweka gemu ya mpira kwenye application hiyo ingawa gemu hiyo haionekani waziwazi(imefichwa). Ili kuweza kucheza gemu hiyo mtuamiaji anatakiwa kufanya mambo yafuatayo:-
-
Kuhakikisha kuwa FB messenger ipo updated na kama haipo updated basi hakisha kuwa unaiupdate
-
Fungua sehemu ya kutuma ujumbe kisha tuma “Soccer emoji” kwa rafiki yako
-
Anza kujiburudisha kwa kucheza gemu hiyo
>Kitu cha kuzingatia wakati wa kucheza gemu hiyo
La muhimu la kuzingatia wakati wa kucheza gemu ni kuhakijisha kuwa unaudundisha mpira na kuweza kulenga emoji zitakazokuwa zinajitokeza ambazo ni za rangi ya dhahabu. Pili, kuhakikisha kuwa unalenga emoji nyingi zaidi na kupata alama nyingi kadri unavyozidi kuendelea kulenga wmoji.
Kucheza gemu kunafanya akili ipumzike kwa namna moja au nyingine, game pia inafurahisha na kuweza kukuondolea huzuni iwapo gemu hiyo itakuvutia na kukufanya uwe na furaha na kuweza kuwa na faraja moyoni mwako. Inashauriwa kupumzisha akili zetu kwa kucheza gemu mbalimbali baada ya kufanya kzai ngumu ambayo imefanya akili yako ichoke.
Tuandikie maoni yako kuhusu makala hii na unaweza kufuatilia Teknokona kupitia Facebook, Instagram na Twitter.
Chanzo:PCMAG.COM na thenextweb.com