Sensa maarufu kutoka Apple ambayo inajulikana kama FaceID, hii ilianza kupatikana kwa mara ya kwanza katika iPhone X mwaka 2017.
Hii haikuishia hapa tuu hata teknolojia hii ilifika mpaka kwa baadhi ya matoleo ya iPad Pro. Ukiachana na teknolojia hii kuweza kutia miguu katika vifaa hivi viwili tuu bado haijaingia katika vifaa vingine vya Apple
Fikiria vifaa kama Mac na vifaa vingine vikubwa zaidi. Lakini teknolojia nyingine ile ya utambuzi wa alama za vidole (fingerprint) wameweza kuuweka hata katika baadhi ya laptop za Mac.
Sasa lakini ndio sensa ya utambuzi (TouchID) pekee ambayo kompyuta kutoka Apple zinamiliki. Nadhani hili sasa linakaribia kubadilika.
Kwa sasa kuna fununu nyingi kwa Apple wataanza kuweka Sensa ya FaceID katika vifaa vyake vikubwa ikiwepo ni kompyuta n.k.
Unajua uwezo wa kutoka loki kwa kutumia FaceID uko na uharaka zaidi kuliko TouchID na hii teknolojia ikifika katika kompyuta kwa kiasi kikubwa itasadia ufunguzi wa kompyuta kwa haraka.
Fikiria kila mtumiaji (user) akawa na uso wake katika komypyuta moja. Hii itarahisisha kazi nyingi sana sio? lakini kingine ni kwamba teknolojia hii inaweza isije kwa haraka kama tunavyodhani
No Comment! Be the first one.