Kampuni ya usafiri wa ndege maarufu nchini ya FastJet ipo njiani kutambulisha ndege yao mpya, ndege hiyo ni Embraer E190.
Kampuni ya ndege ya Embraer ni ya nchini Brazili inayojihusisha na utengenezaji wa ndege za abiria, za kijeshi, kilimo na ata za kutumiwa na makampuni binafsi (mabosi).
Ndege ya Embraer E190 ni toleo lao la ndege la abiria kutoka familia ya ndege za E-Jet kutoka kampuni ya Embraer. Ndege za Embraer E190 zimetengenezwa kubeba kati ya abiria 96 hadi 114 kulingana na chaguo la aina ya viti kutoka kwa kampuni nunuaji.
Ndege ya kwanza ya E190 ilirushwa Februari 19 mwaka 2002, ila kuanzia Machi 2004 ndio ndege ya kwanza ya Embraer E190 ilipokewa na mteja wa kwanza, ambapo ilikuwa ni kampuni ya ndege ya LOT Polish Airlines, ya nchini Polandi.
Ndege hii inauwezo wa kubeba hadi kilogramu 13,047 ya uzito (abiria na mizigo), na ikaweza kuruka hadi umbali wa km 4,537 kutoka usawa wa bahari.
Vyanzo vinaonesha bei ya ndege hiyo ni kati ya dola za Marekani milioni 46.2 (Takribani Tsh Bilioni 103).
FastJet inategemea kuanza kuitumia katika baadhi ya safari zake kuanzia katikati ya Novemba mwaka huu.
Vyanzo: Corporate-digest.com, Embraer na tovuti mbalimbali