Kupitia kipengele hiki kipya kutoka katika mtandao wa kijamii wa Snapchat ni kwamba wazazi watakua na uwezo mkubwa wa kufuatilia watoto wao katika mtandao huo.
Hapa kampuni ya Snapchat imeweka nguvu kubwa katika usalama wa motto, na hapa kilichofanyika ni kwamba wamekuja na kipengele cha uangalizi/usimamizi kinachoitwa Family Center.
Hapa kinachotokea ni kwamba wazazi au hata walezi watakua na uwezo wa kufuatilia mtoto anazungumza na nani katika mtandao huo
Hili linafanyika katika hali ya kwamba mzazi/mlezi hataona ujumbe kamili lakini ataweza kuona tuu mtoto huyo anaongea na nani katika mtandao huo
Ila cha kwanza kabisa kufanyika ni kwamba lazima akaunti mbili ziwe zimeridhia yaaani akaunti ya mtoto na mlezi/mzazi –kinachotakiwa hapa ni upande mmoja kutuma maombi na upande wa pili kukubali maombi hayo.
Hili likishafanyika sasa hapa ndipo mzazi/mlezi ataweza kuona orodha ya marafiki wa mtoto na baadhi ya akaunti ambazo mtoto ameweza kuwasiliana nazo kwa namna moja au nyingine kwa muda wa siku saba.
Kwa kiasi kikubwa kampuni inasema imekuja na kipengele hiki ikiwa ni mahususi kabisa katika dhima yao ya kuhakikisha kuwa usalama kwa watoto katika mtandao wa Snapchat unapewa kipaumbele kabisa.
Hivyo basi kwakua huduma bado ni changa kabisa pengine tutegemee maboresho mengi sana katika kipengele hichi cha Family Center kutoka Snapchat.
Soma Kila Kitu kuhusu Mtandao Wa Snapchat >>HAPA<<
Ningepeda kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hii umeipokeaje? Unaona ni sawa kwa kampuni kuanzisha kipengele kama hicho baina ya mzazi/mlezi na mtoto?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.