Tecno Phantom X ni simu janja ambayo amabayo imeweza kuteka soko kubwa na hata kufikia hatua ya kuweza kwenda mbali zaidi kwenye masoko nyingi nyingi la bara la Ulaya.
Kwa lugha rahisi Tecno wameweza kufurahisha watu hasa kwa maboresho amabayo simu husika imeweza kuja katika hali ya ubora wa hali ya juu. Moja ya vitu ya vitu ambavyo ni vipya kwenye ndugu huyu mpya ndani ya familia ya Phantom ni ubora wa kioo ni Super AMOLED wakiachana na vioo vya LCD. Sifa nyinginezo ni kama ifuatavyo:-
Kioo :
- Ukubwa: Urefu wa inchi 6.70
- Ubora: Super AMOLED (1080*2340px, 90Hz); ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie
Memori :
- Diski uhifadhi: 256GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 8
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 50, 13 na 8+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 48, 8+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu.
Tecno Phantom X: Muonekano wa nyuma na mpangilio wa kamera. Upnde wa mbele/nyuma unalindwa na Gorilla Glass.
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4700 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 33W (70% ndani ya dakika 30 tu)
Kipuri mama :
- Mediatek Helio G95
Uzito :
- Gramu 201
Programu Endeshi
- HIOS 7.6, Android 11
Rangi/Bei :
- Dhahabu na Bluu
- GB 8/256-$460 (zaidi ya Tsh. 1,058,000) bei ya Kenya
Ina redio, sehemu ya kuchomeka spika za masikioni, inatumia kadi mbili za simu, teknolojia ya kutumia alama ya kidole ipo chini ya kioo, mnara wa mawasiliano ni GSM / CDMA / HSPA / LTE, Bluetooth 5.0, WiFi.
Mbali na Afika simu imepenya kwenye masoko ya Columbia, Pakistan, Uturuki na inaonekana kuwa inapata mapokezi mazuri kwa wateja sehemu nyingi suniani. Wewe je, unaionaje?
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.