Facebook imekuwa kiungo muhimu sana katika kurahisisha mawasiliano kwa kwenye Facebook bila hata kufungua app kuu ya Facebook na ukafungua tu Facebook Messenger na ukaweza kujibu ujumbe na hata kupiga/kupokea simu kupitia kwenye Facebook Messenger.
Mbali na kutuma/kupokea ujumbe kwenye Facebook pia mtumiaji anaweza kutuma nyaraka, picha, video na aliyetumiwa akawa na uwezo wa kuona na kufungua kile kilichotumwa lakini kwa kwenye upande wa kutuma/kupokea picha kwenye Facebook Messenger ndio sasa Facebook imeangalia kwa jicho la ziada na kuboresha.
Facebook imebainisha kuwa takribani picha bil. 17 zinasambazwa kila mwezi duniani kote lakini tangu huko nyuma Facebook iliruhusu picha za kiwango cha 2K kuweza kutumwa/kupokelewa. Picha zaubora wa 2K au 4K unategemeana na kifaa (kamera, simu, n.k) iliyopga picha husika.
Katika masasisho ambayo yameanza kupatikana kwenye Facebook Messenger mtumiaji wa Facebook Messenger anaweza kutuma picha iliyo katika ubura wa 4K tofauti na hapo awali ambapo Facebook ilikuwa ikikubali picha za kiwango cha ubora wa 2K.
Tofauti kati ya picha ya kiwango cha 2K na 4K.
Teknolojia inavyozidi kukua na ndivyo vitu vinazidi kuboreshwa na kuleta kitu kitu/mambo mapya kwenye ulimwengu wa teknolojia. Tunapozungumzia picha ya ubora wa kiwango cha 2K au 4K ina maana ya muunganiko wa vipande vidogo vidogo (pixels) ambapo zikiungana kwa pamoja ndio picha kamili inatokea.
Picha ya ubora wa 2K uwiano wake unakuwa ni karibu vipande vidogo vidogo 2,000 huku uwiano wa picha za kiwango cha 4K ukiwa ni 4096 x 4096 pixels. Picha za 4K zina muonekano ang’avu sana kulinganisha na ubora wa picha za 2K. Kujua zaidi kuhusu pixels BOFYA HAPA!
Sasisho hili limeanza kupatikana Marekani, Kanada, Ufaransa, Australia na Uingereza. Kwa nchi nyingine Facebook inatarajia kuruhusu sasisho hilo katika siku za usoni. Vipi umefurahisha na kile kilichoboreshwa kwenye Facebook Meesenger?
Vyanzo: The Verge, Engadget