Mtindo wa watu kutengeneza video fupi fupi kwenye mitandao ya kijamii ni maarufu sana siku hizi kiasi kwamba kuna wengine wameshakuwa na uraibu wa kuperuzi kwenye Facebook Reels, TikTok, n.k.
TikTok amabyo inamilikiwa na kampuni-ByteDance imetokea kuwavutia watu wengi ulimwenguni kote na kiasi kwamba wamejitokeza kudhamini mashindani mbalimbali Afrika na duniani kwa ujumla. Ukubwa wa TikTok ndio uliosababisha makampuni makubwa kama Meta kufikiria na kuja na kitu ambacgo kitaleta ushindani dhidi ya bidhaa ya ByteDance.
Meta ilizindua Reels kwenye Instagram mwaka 2020 na 2021 ikaenda Facebook na kwa mujibu wa kioongozi mkuu wa Meta, Bw. Mark Zuckerberg anasema Facebook Reels ni kitu ambacho kinakua kwa kasi sana na tayari watu wanatumia nusu ya muda wao kuperuzi humo.
Katika kukabiliana na ushindani dhidi ya TikTok, kipengele hicho cha video fupi fupi sasa inapatikana kwenye nchi 150 duniani kote. Kutanuka kwa wigo wa upatikanaji wa Facebook Reels ambapo ni faida hata kwa wale watengenezaji (creators) wa video kuzidi kujitengenezea kipato kupitia kitu hicho kupitia matangazo.
Hatua hii ya inatoa taswira ya kwamba ushindani upo na watu wanatafuta njia sahihi za kukabiliana na mpinzani kwa lengo la kujiongezea kipato na kujikusanyia watumiaji wengi zaidi wa bidhaa husika.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
Elias