Facebook ni moja kati ya mitandao ya kijamii maarufu sana na mkongwe, licha ya kuwa hivyo bado ni moja kati ya mtandao wa kijamii unaoleta ushindani wa juu kwa mitandao mingine sasa wamekuja na ‘Feeds’ Na ‘Home’.
Facebook kwa sasa imefanya masasisho katika mtandao huo hasa katika App yake kwa kuongeza kipengele kipya cha ‘Feeds’…kwa muonekano katika iPhone kipo chini na kwa Android kipo juu
Kipengele hichi cha ‘Feeds’ katika mtandao huu kitakua na kazi kubwa ya kukuonyesha post mbalimbali, na post mpya Zaidi ndio zitakaa kwa juu.
Vitu kama vile zile post ambazo mtandao huo huwa unakua umekuandalia kwa ajili yako (suggested for you) na vitu kama vile matangazo n.k havitakua vikionyeshwa hapa.
Ukurasa wa kwanza kabisa ukiwa unafungua App hiyo ndio utakua unaitwa ‘Home’ na hapa ni tofauti kabsia na katika ‘Feeds’ pengine mambo mengine yote utaweza kuyapata huku.
Sio mara ya kwanza kwa mtandao huu wa kijamii kuja na maboresho au vipengele vipya hivi karibuni tuliandika kuhusu Facebook kuwa na mpangalio mpya wa makundi (group) soma zaidi >>HAPA<<
Soma Kila Kitu Kuhsu Facebook >>HAPA<<
Chanzo: Meta/Facebook
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika uwanja wa comment, je unaona kulikua na haja yoyote kuja na vipengele hivi au Facebook ingebakia vile vile tuu?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.