Je unaweza unaweza kufikiri ni vigumu Facebook kufahamu pale watumiaji wake wanapofanya ngono? Imefahamika si vigumu, na yote yanafanikishwa kupitia mifumo ya data za apps na huduma za matangazo ya Facebook.
Katika apps za sekta ya afya ni apps zinazohusisha mizunguko ya hedhi ndio maarufu zaidi
Shirika linalotetea haki za watu dhidi ya teknolojia za kisasa – Privacy International limetoa ripoti inayoonesha tovuti maarufu ya mtandao wa kijamii ya Facebook kwamba huwa unataka kufahamu hadi maisha ya kingono ya watumiaji wake ili kutumia data hizo kwenye huduma zake za kimatangazo.
Apps za uzazi na kufuatilia mizunguko ya hedhi ni maarufu sana hasa hasa kwa wanawake. Ripoti ya Privacy International inaonesha kupitia teknolojia zake za kimatangazo za Facebook zinazowekwa kwenye apps hizo baadhi ya apps maarufu zimekuwa zikituma (kushare) taarifa za watumiaji wake na hali zao hii ikiwa ni pamoja na masuala ya ngono kwenda huduma ya matangazo na data ya Facebook.
Facebook na Ngono: Mfano hapa PI waliweza kuona data ambayo mtumiaji aliweka kwenye app ambapo taarifa yake juu ya lengo la kutumia app hiyo ilitumwa kwenda Facebook. Lengo likiwa ‘kupata mimba’
Apps za masuala ya uzazi na kufuatilia mizunguko ya hedhi zimekuwa zikihitaji data/taarifa mbalimbali kutoka kwa mtumiaji ili kuweza kutoa ushauri mzuri zaidi kwa mtumiaji. Baadhi ya data hizo zinahusisha tarehe za mizunguko ya hedhi, na pia kama mwanamke anataka ujauzito basi atakuwa anapata ushauri wa siku za kufanya ngono na yeye kukubali (kutick) au kukataa kama tendo hilo halilifanya – kwa kuweka taarifa hiyo kwenye app hizo.
Apps maarufu zilizokutwa zikifanya hivyo ni pamoja na
Maya kutoka kwa Plackal Tech (ina zaidi ya downloads milioni 5 kwenye Google Play),
MIA kutoka kwa Mobapp Development Limited (downloads milioni 1) na
My Period Tracker iliyotengenezwa na Linchpin Health (downloads zaidi milioni 1 Google Play)
Uchunguzi wa Privacy International umekuta data hizo huwa zinatumwa kwenda kwa baadhi ya makampuni ya kimatangazo na hii ikiwa ni pamoja na Facebook. Iwapo mtumiaji amejiunga kwenye app husika kwa kutumia Facebook (login with Facebook) basi Facebook wanakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kumtumia mtumiaji huyo matangazo pale atakapokuwa anatumia huduma za Facebook au za washirika wa Facebook kupitia kurushiwa matangazo yanayohusiana na maisha yake ya kingono kwa wakati huo.
Kwenye app ya Maya ambapo watumiaji huwa pia wanajibu maswali ya ‘Unajisikiaje muda huu’, majibu yao pia yamekuwa yakijumuishwa kwenye data inayotumwa kwenda Facebook
Suala hili ni uvunjifu wa sheria mbalimbali za kimataifa katika mabara ya Ulaya na ata Marekani. Inasemekana muda si mrefu Facebook wanaweza jikuta katika mashtaka kutoka vyombo vya Marekani, Uingereza na Bara la Ulaya (EU).
Suala la ‘Big Data’ – mjumuhisho wa data/taarifa mbalimbali za watumiaji wa intaneti limekuwa changamoto sana kwa sasa. Suala kubwa likiwa ni jinsi gani ya kuhakikisha data za watumiaji wa huduma/mitandao/apps mbalimbali zinakuwa salama na haziendi kutumika nje ya matakwa yao.
Ingawa tayari Ulaya na Marekani wameshaanza kubana huduma mbalimbali za kimtandao kuhakikisha usalama wa data za utumiaji unalindwa bado katika mataifa yaliyoendelea jambo hili haliangaliwi kwa undani zaidi.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Mbunifu na mpenda teknolojia.
Muanzilishi wa Teknokona, TechMsaada na Teknokona Group LTD - WWW.TEKNOKONAGROUP.COM
Muda wangu umegawanyika kati ya kazi kibunifu @teknokonagroup na uandishi wa habari za Teknolojia hapa Teknokona Blog.
| mhariri(at)teknokona.co.tz |