Facebook kuwapa watumiaji uwezo wa kuchagua zaidi kile ambacho kinatokea eneo la nyumbani la huduma hiyo, yaani Timeline. Sehemu inayokupa taarifa ya yanayojiri kutoka kwa marafiki, makundi na kurusa unazofuatilia.
Uamuzi huu unakuja ili kusaidia dhidi ya shutuma za muda mrefu za jinsi mfumo wa kikompyuta (algorithm) umekuwa ukichagua vitu vya kutokea na kutokutokea katika eneo la Timeline la mtumiaji wa app hiyo.
Je, nini kipya kinakuja?
Wanaleta uwezo wa kuchagua aina gani ya mpangilio wa eneo hilo unataka kuangalia. Kutakuwa na;
- Lililopo kwa sasa, mpangilio unaochaguliwa na mifumo ya kimpyuta ya Facebook, algorithm.
- Kihistoria, yaani utaweza kuona habari mpya zaidi juu kutoka kwa marafiki, kurasa unazofuatilia na mazungumzo ya makundi (Groups).
- Kutoka kwa kundi lako binafsi – hapa utaweza kuchagua kurasa, makundi na watu wako wa muhimu ambao hutaki kukosa habari zao.
Facebook wamesema uwezo huo wa kuchagua utakuwa kwa watumiaji wote. Kingine kipya kinacholetwa ni pamoja na kuwapa watu uwezo wa kuchagua nani wa kuwaruhusu kuacha maoni yao kwenye machapisho (post) zao. Hivyo utaweza kuamua kama ni wale uliowaowataja kwenye chapisho tu ndio wataweza kutoa maoni yao, au marafiki au mtu yeyote kwenye tovuti hiyo.
No Comment! Be the first one.