Facebook nao wameona wasibaki nyuma kabisa katika teknolojia ya saa janja. Wametoa muda ambao saa hizo zitaanza kupatikana katika soko mwaka 2022.
Saa hiyo itakua na vipengele viwili vikubwa cha kwanza ikiwa ina uwezo wa kupima mapigo ya moyo na cha pili ni kwamba itakua na uwezo wa kupiga picha.
Picha hizi mtumiaji anaweza akazisambaza moja kwa moja katika mtandao wa instagram na facebook. Kioo cha saa janja hii kitakua na kamera mbili.
Kioo hicho pia kama saa janja nyingi ni kwamba kina uwezo wakuchomoka na kurudi katika mikanda yake, na kikichomoka ndipo hapo mtumiaji anaweza akaanza kuchupiga picha hizo.
Facebook wao wanasema wanajikita katika kuleta vifaa vya kielekroniki ili kuweza kuleta ushindani na ikibidi kuwapita wapinzani wengine na hivyo kusaidia au kukuza soko lao maana watumiaji watakua wanapata kile kilicho bora zaidi.
Saa itakuja katika rangi za nyeusi, nyeupe na gold. Vile vile Facebook watakua wanatumia teknolojia walionunua katika kampuni ya CTRL-labs ambayo inajihusisha sana na vifaa vya kielektroniki vya mkononi.
Ni kweli Facebook hawana historia nzuri na vifaa (vinavyoshikika) kwani kuna matoleo ya vifaa kadhaa waliachia lakini bado havikufanya vizuri sokoni.
No Comment! Be the first one.