Facebook kubadilisha jina na kubeba jina litakalokuwa jumuishi kuwakilisha bidhaa zote zilizopo chini yake, hii ikiwa ni pamoja na mtandao wa kijamii wa Facebook, Instagram na huduma zingine nyingi kuwa sehemu tu ya kampuni hii mpya.
Inaonekana Facebook wanachukua uamuzi ambao Google mwaka 2015 kupitia ujio wa kampuni ya ALPHABET walifanya. Facebook inafahamika zaidi kama Facebook – mtandao wa kijamii, ila kwa sasa kampuni ya Facebook inamiliki huduma na kampuni zinazotengeneza bidhaa ambazo hazina mahusiano ya moja kwa moja na mtandao wa kijamii wa Facebook.
Kwa sasa kampuni ya Facebook, nje ya kumiliki mtandao wa kijamii wa Facebook ina miliki pia huduma zingine kama vile Instagram na Whatsapp.. Pia ilishanunua makampuni mengine 76 katika kipindi cha miaka 15 iliyopita.Hatua ya kubadili jina la kampuni mama – kampuni itakayokuwa ndio inayosimamia na kumiliki makampuni mengine yote hii ikiwa ni pamoja na mtandao wa kijamii wa Facebook imechukuliwa kama ni hatua sahihi na itasaidia katika usimamizi na uendeshaji wa makampuni hayo.
Baadhi ya manunuzi makubwa zaidi kufanywa na Facebook. Kumbuka $ bilioni 1 ni zaidi ya Tsh Trilioni 2.3.
- WhatsApp ($19 b)
- Oculus VR ($2 b)
- Instagram ($1 b)
- CRTL-labs (Kati ya $500,000,000 na $1 b)
Hadi sasa jina jipya la kampuni ni siri kubwa ambayo ipo kwa watu wachache tuu wa uongozi wa juu zaidi katika kampuni hiyo. Ila tutegemee kufikia mwisho wa mwezi huu kwenye tukio la Facebook la kufunga mwaka kuna uwezekano pia utambulisho huo utafanyika.
Vyanzo: Titlemax na Google News
No Comment! Be the first one.