Kampuni ya utafiti inayoheshimika nchini Marekani, eMarketer, imesema Facebook inapoteza vijana Marekani wakati app ya Snapchat inazidi kuvutia vijana wengi zaidi.
Kampuni ya eMarketer mwanzoni mwa mwaka jana ilitabili ya kwamba mtandao wa Facebook utapoteza asilimia 3.4 ya watumiaji wa umri wa kati ya miaka 12 hadi 17 kufikia mwisho wa mwaka 2017, data zinaonesha mtandao huo umepoteza watumiaji wengi zaidi ya utabiri huo wa eMarketer.
Kwa mwaka 2017 mtandao wa Facebook umepoteza asilimia 9.9 ya watumiaji wake wenye umri wa kati ya miaka 12 hadi 17 nchini Marekani, yaani takribani watumiaji milioni 1.4.
Kwa mwaka 2017 idadi nzima ya watumiaji wa mtandao huo wenye umri wa miaka 12 hadi 17 nchini Marekani ilikuwa ni milioni 12.1.
Mtandao wa Snapchat unazidi kuwa ndio rafiki zaidi kwa vijana nchini humo.
Kwa Marekani mwaka 2018…
- Snapchat itaongeza watumiaji milioni 1.9
- Instagram itaongeza watumiaji milioni 1.6
Kwa mwaka 2017 Facebook ilipoteza watumiaji milioni 2.8 kwa kundi la chini ya miaka 25 nchini Marekani, shirika la eMarketer limesema kwa mwaka huu watapoteza tena watumiaji milioni 2.1 katika kundi hilo.
Je wewe unaitumia app ya Snapchat na pia ni mtumiaji wa Facebook? Unamtazamo gani juu ya mitandao hii mitatu ya kijamii? Upi unautumia zaidi?
Chanzo: eMarketer