Emoji ni picha au nembo inayopachikwa katika maandishi na kutumika katika jumbe za kielektroniki pamoja na kurasa za tovuti. Kuna aina mbalimbali za emoji kama emoji za sura, vitu vya kawaida, maeneo, aina za hali ya hewa na wanyama.
Neno Emoji limetoka kwenye lugha ya Kijapan “e (picha)+Moji (barua/mchanganyiko wa herufi na namba)” likiwa na maana ya picha. Emoji zilianza kutumika katika simu za wajapan mwaka 1997 na kupata umaarufu zaidi mwaka 2010 zilipoanza kutumiwa na kampuni za watengeneza simu. Kuna zaidi ya Emoji 3000 zinazotumika mpaka sasa. Emoji hutumiwa na watu kujieleza, kukuza mwingiliano katika maongezi na kuonyesha hisia kwa njia ya ujumbe.
Emoji 10 na maana zake
Emoji zina maana tofauti tofauti kulingana na nchi uliyopo, imani pamoja na utamaduni wa eneo ulilopo au mtu unayewasiliana nae. Zifuatazo ni baadhi ya Emiji pamoja na maana zake.
- 😂- Emoji hii humaanisha kucheka sana hadi kulia lakini muda mwingine hukosewa na kutumika kama Emoji ya kulia.
- 😎 – Emoji hii hutumika kuashiria kujiamini.
- 😇 – Emoji hii huashiria kuwa na amani au kubarikiwa.
- 🙃 – Emoji hii hutumika kuonyesha kuwa umefurahi lakini huna furaha.
- 🙇 – Emoji hii hutumika Japan kuashiria kuabudu lakin. pia watu huitumia kuashiria kufikiria kwa kina.
- 🤦♀️ – Emoji hii huweza kutumika kuashiria kichwa kuuma, kuona aibu au kusahau kitu cha muhimu.
- 😶 – Emoji hii hutumika kuashiria kuwa umekosa cha kusema au huwezi kuchangia mada.
- 🙌 – Emoji hii humaanisha kukubali hali au kutojali kuhusu kitu.
- 🖐 – Emoji hii humaanisha kusimamisha jambo lisiendelee.
- 🙏 – Emoji hii huashiria watu kugonga mikono hewani na pia katika tamaduni zingine humaanisha kusali.
No Comment! Be the first one.