Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya magari yanayotumia mfumo wa umeme ya Tesla, amesema walishajaribu kuwauzia Apple kampuni ya Tesla ila Tim Cook alizingua. Inasemekana kwa wakati huo kampuni ya Tesla ilikuwa kwenye changamoto mbalimbali.
Kama Apple wangekubali kufanya mazungumzo na Bwana Elon Musk na kununua kampuni hiyo basi wangekuwa kifua mbele kwenye teknolojia ya magari, kampuni ya Tesla ina thamani ya mara 10 zaidi ukilinganisha na bei ambayo Elon Musk alitaka kuwauzia kipindi hicho.
Inasemekana tayari Apple wameaanza uwekezaji ili kujiingiza katika biashara ya utengenezaji na uuzaji wa magari ya kisasa yanayotumia Umeme. Ila kwa sasa tayari Tesla ndio kampuni iliyo juu zaidi kwenye teknolojia hiyo, ikitoa ushindani mkubwa ata kwa makampuni mengine makubwa ya muda mrefu kama vile Toyota na General Motors.
Kulingana na taarifa za chombo cha habari cha Reuters, Apple wanategemea kutambulisha gari lao la kwanza ifikapo mwaka 2024. Kama watafanikiwa au hapana, bado ni mwanzo sana kufahamu kwa kuwa ndio kwanza vyanzo vya uhakika vimeanza kutoa taarifa juu ya malengo hayo ya Apple.
Kampuni ya Tesla kwa sasa tayari imejiweka vizuri kwenye soko na inatambulika kama kampuni iliyo na teknolojia za kisasa katika mfumo mzima wa magari yake – uwezo wa kwenda kilometa za mbali kwa kuchaji, uwezo wa kujiendesha yenyewe bila uhitaji wa dereva nk.
Hakika itakuwa mkurugenzi wa Apple, Bwana Tim Cook anajutia kiasi flani uamuzi wake wa kutokubali kikao na Bwana Elon Musk pale alipoonesha nia ya utayari wa kuuza kampuni ya Tesla kwao miaka kadhaa nyuma.
Chanzo: Yahoo
No Comment! Be the first one.