Maana ya kampuni kuwa kwenye soko la hisa ni kwamba sasa umiliki wake sio tena wa binafsi bali umma hivyo mtu yeyote mwenye uwezo anaweza akanunua hisa na kuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni husika.
Baada ya miaka mitano kuwa katika umiliki binafsi Desemba, 28 2018 DELL ilirudi kwenye soko la hisa na hisa moja ilikuwa ikiuzwa $46 na kupanda baada ya muda kidogo.
Mwaka 2013, mwanzilishi na Afisa Mkuu Mtendaji, Bw. Michael Dell aliamua kuifanya kampuni hiyo kuwa ya binafsi tena kwa gharama ya $25bn kwa ushirikiano na kampuni nyingine, Silver Lake.
Katika kipindi cha miaka mitano ambayo DELL ilikuwa ikimilikiwa kibinafsi ilipata faida kutokana na mauzo ya kompyuta mahususi kwa ajili ya kucheza magemu, huduma za utuzaji vitu sehemu isiyojulikana.
Vyanzo: The Verge, Forbes