Baada ya kukifunga kiwanda chake kimoja kwa muda kutokana na Corona, Nokia waliamua kukifungua tena hivi karibuni kutokana na maambukizi kupungua. Wiki hii wamejikuja wakikifunga tena kiwandao hicho baada ya wafanyakazi wengine 42 kukutwa na maambukizi ya Corona.
Kiwanda hicho cha vifaa vya mawasiliano kinachomilikiwa na Nokia kipo kusini mwa jimbo la Tamil Nadu nchini India. Kiwanda kilikuwa kimefungwa kwa muda mrefu kuendana na sera ya serikali ya kusimamisha shughuli za kiuchumi na za kijamii kama njia ya kupambana na Corona.
Nokia walifungua kiwanda hicho tena hivi karibuni baada ya sheria kulegezwa baada ya kuonekana maambukizi ya Corona yameporomoka katika eneo hili. Kufunguliwa kuliendana na kuendelea kuwapima wafanyakazi mara kwa mara na ndio imeonekana kuna ulazima wa kufunga tena kiwanda hicho kwani bado maambukizi yanatokea kwa wafanyakazi wake.
Janga la Corona limeathiri sana viwanda vinavyohitaji wafanyakazi wengi kwa ajili ya kazi zake. Katika kipindi hicho hicho makampuni yanayotengeneza roboti wanaoweza kusaidia kazi mbalimbali za viwandani wanaendelea kutishia upotevu wa ajira nyingi za watu ata baada ya janga la Corona kuisha.