Karibu Teknokona kwa mara nyingine, leo nimekuandalia makala fupi inayohusu kugeuza kompyuta yako kuwa kifaa kinachosambaza intaneti kwa vifaa vingine kama vile simu n.k.
Kwa jina la kitaalamu huduma hii inaitwa hotspot ambapo kumpyuta yako itakua ni kama router. Kuna njia tuliiandikaga hapo kipindi cha nyuma lakini hii ya sasa ndio nzuri zaidi.
Programu ya Connectify Hotspot itakuwezesha kutumia intanet ya kwenye kompyuta yako (kwa mfano kama umechomeka modem) katika simu janja yako. Kitachotakiwa kufanya ni kuwasha WiFi katika simu yako.
Fuata Njia Hizi Kufanikisha Hilo
- Cha Kwanza Kabisa Itakubidi Ushushe Na Ipakue Programu Hiyo Hapa.
- Baada ya kuipakua na Kufuata maelekezo yote ya kuipakua (Chagua ile ya toleo bure kama huwezi Kulipia).
- Ikishajipakua ifungue na kisha na kisha anza kujaza sehemu ya jina lako unalotaka kulitumia katika Hotspot na NenoSiri ambalo litahitajika kwa wale wataotaka kujiunga katika Intaneti huiyo kuputia WiFi.
- Ukimaliza hilo chagua Start Hotspot.
- Mpaka hapo unaweza ukachukua simu yako na kuanza kutumia Hotspot (intanet) ya kwenye kompyuta yako moja kwa moja katika simu yako.
- Wale wanaotumia Windows za zamani kama vile Window XP na Window Vista wanaweza wasipate huduma hii hivyo ni vyema kupata toleo jipya zaidi la Windows.
Mimi natumia Windows 10 na mpaka sasa naifurahia huduma hii. Katika program hii huduma ya WiFi Hotspot ndio ya bure pekee ila huduma ya Wired Router na WiFi Repeater ni za kulipia. Pia unaweza ukabadilisha settings zako mara kwa mara (wewe ndio bosi) na pia unaweza ukatembelea eneo la Clients ili kuangalia vifaa vinavyotumia intenet yako kupitia WiFi