Shirika la Utafiti wa Anga za Juu la Marekani, NASA, lipo katika hatua za mwisho za kutuma choo cha thamani ya zaidi ya bilioni 53 za Kitanzania kwenda katika kituo cha anga cha kimataifa kilicho katika anga za juu.
Choo hicho chenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 23, ni choo kinacholenga kuja kutumika hadi kwenye kituo cha anga kitakachokuja kujengwa mwezini.
Choo hichi ni kidogo kwa asilimia 65% ukilinganisha cha sasa kilichopo katika kituo cha anga cha kimataifa (International Space Station). Pia ni chepesi kwa asilimia 40%. Katika masuala ya anga wepesi na udogo kwa vifaa muhimu ni mambo muhimu sana kwani kupeleka vitu vizito angani ni ghari sana na pia kwa ufanisi kituo hicho cha anga ni muhimu uzito wake usiwe unaongezeka sana.
Sifa za Choo
- Kina uwezo wa kuchukua unyevu nyevu wa vinyesi vikubwa na vidogo na kisha kuzalisha tena maji safi yanayoweza kutumika tena.
- Kina uwezo wa kuvuta kinyesi kwa kutumia nguvu ya hewa na hivyo kuweza kuepusha ajali za uchafu kwani katika kituo cha anga hakuna nguvu ya mvuto kama ilivyo huku duniani (gravitational force).
- Kiti chake kitaweza kutumiwa vizuri kuliko cha sasa ambacho hakikuwa bora sana, hasa kwa wanawake. Kiti cha choo cha sasa ni kama vile vya vyoo vya kukodi kwenye matukio.
Choo hicho kitasafirishwa katika chombo cha safari za anga siku ya Jumanne, Septemba 29, kwenda kwenye kituo cha kimataifa cha tafiti za anga.
Kwa habari zingine za anga tembelea -> Teknokona/anga
No Comment! Be the first one.