Chombo cha anga cha Ulaya kinachokwenda kwa jina la Schiaparelli kinatarajiwa kutua katika sayari ya Mars.
Chombo hicho kimefanikiwa kujitenga na “chombo mama” angani na kwa sasa kinaelekea kwenye sayari ya Mars.
Chombo hicho kinatarajiwa kujaribu kutua kwenye sayari hiyo Jumatano na kina uzani wa kilo 577. “Schiaparelli” ilifanikiwa kujitenganisha na chombo mama Jumapili saa kumi na moja jioni saa za Afrika Mashariki.
Schiaparelli ni kifaa cha kufanyia majaribio teknolojia, na lengo kuu ni kudhihirisha uwezo wa Shirika la Anga za Juu la Ulaya (ESA) kutua katika sayari hiyo.
Chombo hicho kitakuwa na muda wa chini ya dakika sita kupunguza kasi yake ya kilomita 21,000 kwa saa kiasi cha kukiwezesha kutua salama kwenye sayari hiyo.
Jaribio la awali la shirika hilo kutua katika sayari hiyo lilifanyika mwaka 2003, kwa kutumia chombo cha Uingereza cha Beagle-2. Chombo hicho kilifanikiwa kutua salama lakini kikashindwa kufungua mitambo yake ya kawi ya jua vyema na hivyo mawasiliano yakakatika
Baada ya muda mambo yalikaa sawa na kuweza kutumia kufanya uchunguzi wake. Una lolote la kutuamia? Tuamdikie katika sehemu ya comment. TeknoKona ipo pamoja nawe kila siku.
Vyanzo: BBC