Katika moja ya vitu ambavyo teknolojia inayokuwa na kuendelea kuvutia na soko la ushindani basi sarafu za kidijiti zipo na zinaendelea kubuniwa kila leo, Tanzania zipo kadhaa na mojawapo ni Diligence.
Moja ya sababu ya mambo kwenda sawia/kama ilivyotarajiwa ni baada ya kufanyika utafiti wa kina kabla ya kuanza kutumika na ni hivyo hivyo kwa sarafu ya kidijiti, Diligence.
iRA ni nini?
iRA (incentive Research Africa) ni mpango ambao unahusisha masuala ya utafiti. Utafiti huo unafanyika kwa njia ya mtandao (online) ukihusisha mambo ya kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiteknolojia barani Afrika.
Deligence ni nini?
Diligence ni sarafu ya kidijitali ambayo itakuwa ikiupa nguvu mfumo wa iRA kama njia ya malipo. Imetengenezwa katika mfumo wa Ethereum. Kuna sarafu za Diligence mil 21 tuu.
Kwa nini iRA?
?Kutambua umuhimu wa mtu anayefanyiwa utafiti na kuufanya utafiti kama moja ya kazi zinazoingiza kipato.
?Watu wengi watashiriki utafiti ndani ya mda mfupi na kupata matokeo sahihi
?Itazuia upikaji wa taarifa za tafiti.
?Mtu atakayeshiriki hizo tafiti atalipwa kwa sarafu ya kidijitali ijulikanayo kwa jina la Diligence.
iRA itafanyaje kazi?
iRA itamtambua kila mtumiaji kwa kumjua kila mteja wake ambapo kutokana na kuwa na kanzi data ya iRA. Taarifa za mtumiaji zitahifadhiwa salama ili kusaidia tafiti zinazokuja ziwafikie walengwa.
Kila tafiti inayokuja itawafikia wahusika tu.
?Mtu ataletewa maswali na atayajibu mtandaoni na baada tu ya kuyajibu atatuma na ajili ya uhakiki.
?Mtu akishamaliza kujibu maswali atalipwa sarafu ya Diligence Maana ndani ya iRA kutakuwa na mfuko wa kidijitali wenye uwezo wa kuitunza sarafu ya iRA. Hivyo, baada tu ya kazi ya kujibu maswali mtu atalipwa.
Hatua iliyopo iRA kwa sasa.
Kuuza asilimia 40 ya sarafu za Diligence duniani kote ili kupata hela ya kuendesha mipango yake ambapo mauzo ya sarafu Diligence yameanza Desemba, Mosi 2018 hadi Februari, 28 2019.