Imekuwa ni rahisi watu kutumiana picha ndani ya kitufe cha kamera kwa njia ya WhatsApp na hii inatokana na jinsi ambavyo programu tumishi imetengenzwa. Kwa wanaotumia iOS mambo yalibadilishwa kidogo lakini sasa vitu vimerejea kama ilivyokuwa hapo awali.
Tunafahamu ilivyo rahisi kiasi gani kumtumia mtu picha kwenye WhatsApp na kuweza kumfikia mara moja kama yupo hwani na mtandao wa intaneti upo vizuri lakni kuna mabadiliko ambayo WhatsApp iliyapeleka kwa wale wanaotumia iOS na kufanya watu watoe ya moyoni kuhusiana na hicho ambacho kilikuwa kimebadilishwa.
Hapo awali WhatsApp walibadilisha mrindo wa mtu kuweza kuchagua picha mara baada ya kubonyeza kitufe cha “Kamera”; picha ambazo zipo kwenye simu zilikuwa hazionekani katika mstari mmoja kutoka kushoto kwenda kulia badala yake kiliwekwa kitufe kimoja tu ambacho kinaonyesha picha moja ambapo ndani yake ndio zipo nyingine. Kitu hicho kililalamikiwa na watumiaji wa WhatsApp kwenye iPhone na walioitengenza kuamua kurudisha kama ilivyokuwa zamani.
Maboresho hayo kwa wanaotumia iPhone hayawezi kuonekana iwapo kama hautaauma kupakua masasisho mpya (kutumia toleo la karibuni kabisa la WhatsApp). Hivyo, ni jukumu lako sasa kuweza kufanya kinachohitajika.
Usisahau kutufuatilia kila siku ili kuweza kufahamu mambo mbalimbali yanayohusu teknolojia kwani tupo hapa kwa ajili ya kukuhabarisha.
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.