Kampuni ya ByteDance, wamiliki wa app maarufu ya TikTok wamesema bado watabaki na umiliki wa teknolojia muhimu ya app hiyo ata baada ya kukubali kuuza sehemu ya kampuni hiyo nchini Marekani kwa Oracle na Walmart.
Tuliandika kuhusu makubaliano hayo ambayo yanaifanya kampuni ya TikTok kuungana na Oracle na Walmart katika utengenezaji wa kampuni mpya inayokwenda kwa jina la TikTok Global. Katika kampuni hii mpya Oracle na Walmart watamiliki asilimia 20 ya kampuni hiyo.
Majukumu ya Oracle:
- Uhifadhi na usalama wa data za watumiaji wa Marekani na mataifa mengine ukitoa Uchina na
- Kuangalia kodi-jenga (source code) ya app ya TikTok mara kwa mara kuhakikisha kuna usalama dhidi ya udukuaji
Teknolojia ya algorithm:
ByteDance wamesema katika makubaliano yao bado ni wao tuu ndio watabaki na siri ya teknolojia kuu ya jinsi aina za post za watumiaji wake zinasambazwa kwenye app hiyo na utumiaji wake.
Teknolojia kuu ambayo watabaki nayo inatambulika kitaalamu kama ‘algorithm’ na ni moja ya teknolojia muhimu zaidi katika mitandao ya kijamii. Inasimamia jinsi gani unaona vitu ambavyo vinatokea pale unapoingia kwenye tovuti husika, kwa kuweza kukuletea posts nzuri basi wanahakikisha unaweza kutumia zaidi tovuti hiyo.
No Comment! Be the first one.