Uimbaji wa nyimbo mbalimbali wakati mtu anapofanya kazi ngumu mathalani bustanini/shambani kwa karne imekuwa kama motisha ya kumfanya mtu aweze kuendelea na kazi yake bila kuhisi kuchoka kwa muda mrefu tu ila kwa mapinduzi ya teknolojia hivi sasa kuna bustani janja yenye sauti nzuri.
Kwa karne zinavyozidi kwenda ndio teknolojia nayo inavyozidi kwenda mbali zaidi kwa watu kuweka fikra na mawazo yao na kuja na vitu vipya kwa ajili ya manufaa ya wengi kwa ujumla. Ulishawahi kusikia kuhusu bustani ya kidigitali?! Ndio, bustani hiyo ipo na hivi karibuni imewekwa kwenye maonyesho huko Tokyo, Japani.
Yote kuhusu bustani ya kidigitali iliyopendezeshwa na teknolojia.
Bustani ipo katikati ya jiji la Tokyo ambayo imetokea kuwavutia wengi kutokana na kile ambacho mbunifu wake, Bw. Ray Kunimoto amekifanya kwenye bustani hiyo ya kijanja ambayo inavutia sana. Bustani hii inapendezeshwa na taa na sauti mbalimbali ambazo zinazunguka bustani nzima (kama kilimo cha greenhouse).
Kwa kugusa tu mmea fulani basi itatoka sauti ya mmea husika mathani pale sauti inayotokana na kucuma chugwa mtini huku taa zenye rangi mbalimbali zikienda pamoja na mlio kutokana na mmea ambao mtu ameushika.
Sauti ambazo zinatoka baada ya mmea fulani kuguswa zinatokana na kurekodiwa kwa sauti halisi ya pale mtu anapokwenda shambani kuchuma tunda/mboga za majani, sauti inayotokana na kutafuna kitu mdomoni, sauti inayotokana na kugusanisha majani/kusugua mbegu na kisha kompyuta kutumia kutengeneza melody saba.
Kila mmea ambao utashikwa utatoa sauti ya aina yake bila kujirudia zikiwemo sauti mbalimbali za ala za muziki mfano tarumbeta.
Mpaka hivi sasa bustani hiyo imetokeea kuwavutia wati mbalimbali wanaotembelea eneo hilo na kuweza kujionea uzuri wa bustani ya kidigitali ambayo itaendelea kuonyeshwa mpaka Novemba 5 2017. Je, unaizungumziaje bustani hii ya kidigitali?
Vyanzo: Colossal, Engadget