Machi 2020 Bw. Bill Gates alijiuzulu nafasi yake kwenye bodi ya wakurugenzi wa Microsoft bila kushikizwa lakini kumbe nyuma ya pazia baadhi ya wajumbe walishamuona hatoshi kuendelea kuwa mmoja wao.
Ni zaidi ya mwaka sasa bilionea Bill Gates si mmoja wa wakurugenzi kwenye bodi ya Microsoft kufuatia kujiuzuu kwake Machi 2020. Wengi wanaamini kuwa hatua hiyo ilitokana na yeye kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na aliyekuwa mhandisi kwenye kampuni hiyo.
Mwaka 2019, bodi hiyo ya ilitafuta kampuni inayoshughuliikia masuala ya sheria na kuipa kazi ya kuchunguza kufuatia malalamiko kwa bodi kupitia barua aliyokuwa ameiandika aliyekuwa mhandisi ndani ya Microsoft akieleza kuwa alikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na Bw. Bill Gates kwa miaka mingi tuu.
Haikufahamika kama kweli barua hiyo aliiona Bi. Melinda na mara baada ya suala hilo kufika juu kabisa bodi ikaagiza uchunguzi ufanyike dhidi ya malalamiko yalikuwa yasemwa na aliyekuwa mfanyakazi wa Microsoft.
Wakati uchunguzi unaendelea baadhi ya wajumbe walishatoa yao ya moyoni na kusema kuwa mlengwa hatoshi kuwepo miongoni mwao tena ingawa hayakuwa maamuzi kwani kampuni iliyokuwa imepewa jukumu la kutafuta ukweli wa suala hilo ilikuwa bado haijakamilisha kazi yake.
Hata hivyo, msemaji wa Bw. Bill Gates alikubali kuwa yalikuwepo mahusiano ya kimapenzi miaka ya 2000 lakini yakaisha kwa amani kabisa. Na suaala la kung’atuka madarakani alikuwa ameshaliwaza miaka mingi nyuma kabla ya hata hicho hicho kilicholetwa machoni pa watu kutokea kwani alihitaji kuangalia zaidi shughuli zake nyingine.
Je, unaizungumziaje habari hii? Tupe maoni yako na kumbuka kutembelea tovuti yetu kila siku kwa habari mbalimbali za teknolojia.
Vyanzo: The Guardian, The verge
No Comment! Be the first one.