Tanzania ukiilinganisha na Uganda/Kenya kuhusu uelwewa wa teknolojia inayowezesha miamala salama kuhusu suala zima la sarafu za kidijitali tupo nyuma lakini kwenye kongamano la pili (AIPC 2018) Blockchain Tanzania watatuelimisha siku hiyo.
Kama moja kati ya wale watu wanaosubiri kwa shauku kubwa kuweza kuhudhuria kongamano la kila mwaka kwa wadau na wana TEHAMA nchini Tanzania, namuomba mwenyezi Mungu anisaidie nisiweze kukosa hata siku moja ili niweze kusikia ambayo yapo, yanayoendelea kwenye teknolojia kwa upana wake.
Mtoa mada siku hiyo ni Jumuiya ambayo imeazimia kuwafanya Watanzania waweze kuelewa, kuamini na hata kuwekeza kwenye upande huo wa teknolojia ambao unaonekana kuvutia mataifa mengi duniani.
Siku ya 2/3 itakuwa ni kuhusu kufahamu mengi ambayo Jumuiya kufahamisha umma wa Tanzania kuhusu teknolojia/uwekezaji kwenye sarafu za kidijitali.
Naamini siku hiyo kwa tutakohudhuria tutajifunza mengi na pengine kuanza kuwekeza kwa mipango ya muda mrefu. Hata hivyo, TeknoKona imealikwa hivyo tutawahabarisha kama kawaida yetu.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|