Tajiri namba moja duniani na pia mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft amejiunga rasmi na mtandao wa Instagram akiwa nchini Tanzania.
Bill Gates akiwa ni mmoja wa watu mashuhuri zaidi katika sekta ya teknolojia alikuwa bado hajajiunga na mtandao wa kijamii wa Instagram.
Uamuzi wake wa kujiunga katika mtandao huo akiwa nchini Tanzania umekuwa wa faida kwa nchi yetu kwani vyombo vya habari vya kiteknolojia vikubwa duniani kote vimeripoti jambo hilo, huku vichwa vya habari vingi vikiwa ni ‘Bill Gates ajiunga mtandao wa Instagram akiwa nchini Tanzania’.
Kwa kiasi kikubwa tunategemea Bill Gates kutumia akaunti yake kwa ajili ya kuonesha shughuli zinazohusiana na shirika lake la misaada ya kijamii – Bill & Melinda Gates Foundation.
Je unataka kujua mengi kuhusu maisha yake na teknolojia?