Bidhaa mbalimbali za kidijiti ambazo zinakujika zimeendelea kujitokeza kwa makampuni makubwa kama Samsung wameendelea kutegeneza vitu vilivyo katika muundo huo.
Mwezi Mei tangu tarehe 17 hadi 21 2021 yamedanyika maonyesho ya kibiashara mahususi yanayolenga vioo ya kidijiti (SID-Society for Information Display) ambapo Samsung iliweza kuonyesha bidhaa zake mbalimbali ambazo inategemea kuzitoa. BIdhaa zenyewe hazina majina rasmi lakini zina uwezo wa kukunjika/kukunjuka.
Mosi, simu janja iliyotengenezwea na Samsung ikikunjuliwa kioo chake kina urefu wa inchi 7.2, kamera za mbele zinaonekana kuwa upande wa kushoto lakini pia ina uwezo wa kukunjika na kuonekana katika pande mbili.
Pili, Samsung waliweza kuonyessha simu janja nyingine iliyotengezwa katika muundo wa kukunjika na kujikunjua, umbo lake ikikunjwa ina ukubwa sawa na rununu nyingi ambazo tunazijua lakini simu hiyo inaonekana kumuwezesha mtu kufanya kitu zaidi ya kimoja kwa wakati huohuo.
Tatu, bidhaa nyingine iliyokatika mtindo wa kukunjika na kukunjuka ni kioo cha urefu wa inchi 17 kinachokunjika nusu. Bidhaa hii inafanana sawa na Surface Neo ya Microsoft halikadhalika Lenovo ThinkPad X1 Fold.
Mwisho lakini si kwa uchache kwenye maoneyesho hayo Samsung walionyesha kipakatalishi wakilenga zaidi kioo ambacho kilionekana kuwa na kamera iliyojengewa ndani kwa ndani hivyo inaaminika kuwa mwaka huu pia kampuni hiyo itatoa kompyuta yenye nakshi naksi za kuvutia.
Bidhaa hizo zinadhihirisha kuwa Samsung bado wanazidi kuongeza idadi ya bidhaa zilizo katika muundo wa kukunjuka na kukunjika. Tupe maoni yako ewe msomaji wetu kuhusiana na hicho ambacho Samsung wameweza kukionyesha kwenye maonyesho.
Vyanzo: GSMArena, The Verge, GizMoChina
3 Comments