Apple wamekuwa wakifanya biashara ya kutengenezewa vioo vya kutumika kwenye bidhaa zao na moja washirika wakubwa ni LG.
Kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa na Electronic Times imeonyesha kuwa LG wanashika nafasi ya pili kwenye kuwatengenezea Apple vioo vya OLED na kabla ya hapo Samsung ndio alikuwa akiwatengenezea kampuni husika (Apple).
Biashara ya vioo kati ya Apple na LG inatazamiwa kushamiri hasa baada ya bidhaa hiyo kutoka LG kushinda vigezo vya kampuni nguli ili kuweza kufanya nao kazi.
Samsung alikuwa ndio yupo mbele kwani alishakubaliana na Apple atengeneze vioo vya OLED takribani 100 milioni kwa idadi na kioo kilichotumika kwenye iPhone X mwaka 2017 kilitengenezwa na Smasung.
Ujio wa LG unaifanya Apple kupunguza utegemezi kutoka upande wa pili hasa kutokana na teknolojia ya vioo ambavyo vinaweza kukunjika.
Vioo ya OLED kutoka LG vinaonekana kuwavutia wengi kwani hata kwenye Google Pixel 2 XL kampuni hiyo inahusika kuwatengenezea Google.
Vyanzo: Reuters, The Verge
One Comment
Comments are closed.