Kwa karibu miaka mitatu sasa duniani bado inapambana na janga la Virusi vya Corona ambalo bado linaendea kuitafuta dunia ingawa sasa tumeshaliona kuwa ni virusi kama virusi vingine tuu.
Ulazima wa kuvaa barakoa kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo ofisini imekuwa ni sehemu ya vazi la mtu kwa muda wote ambao yupo kazini lakini hata kwenye vyombo vya usafiri. Kama njia ya kukabiliana na janja ka la virusi vya Corona Apple ni mojawapo ya makapuni ambayo ilikuwa ni lazima kwa wateja wanaotembelea maduka yao basi wawe wamevaa barakoa lakini sasa wamelegeza masharti.
Kwa mujibu wa sera yao kuhusiana na janga la virusi vya Corona sasa si lazima kwa wateja wanaotembelea maduka yao kuwa wamevaa barakoa ilimraadi tu wawe wamepata dozi ndima ya chanjo ya virusi hivyo.
Majimbo mengi tuu hivi sasa nchini Marekani (Kansas, Ohio na Carolina Kaskazini) si lazima kwa wakazi kuvaa barakoa. Vilevile, maeneo mbalimbali ya New York ambapo maduka ya Apple yapo hayalazimishi wateja wanaokwenda hapo kuwa wamevaa barakoa ingaw bado wabahimiza watu kuvaa barakoa na iwapo mteja hana na akihitaji wanampatia.
Ingawa si lazima kwa wateja kuvaa barakoa wanapotembela maduka ya Apple lakini wafanyakazi wake wataendelea kuvaa mpaka hapo maelekezo kutoka juu yatakapokuwa tofauti.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.