Dunia nzima inafahamu kinachoendelea nchini Ukraine na namna gani wananchi wake wanavyotaaibka kutokana na kilichowakumba. Katika kuishinikiza Urusi iache vita na Apple waombwa kufunga App Store.
Inapotokea vita wananchi, shughuli za maendeleo na mambo megine mengi tuu yanaathirika na hivyo kusababisha uharibifu wa vitu, makazi lakini mbaya zaidi kushuka kwa uchumi kutokana na kwamba hakuna shughuli za uzalishaji zinazofanyyika. Hivi sasa Ukraine imebaki na wananchi wachache sana na hawafanyi kazi kutokana na kile ambacho kinaendelea nchini humo.
Apple ni moja ya makampuni ya teknolojia ambayo yanafanya biashara nchini Urusi na kwa hili ambalo imeamua (Urusi) kufanya sio kitu cha kiungwana na vikwazo mbalimbali vinawekwa kushinikiza nchi hiyo kuacha vita. Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni waziri wa Mabadiliko ya Teknolojia, Bw. Mykhailo Fedorov amemuandikia barua Mtendaji Mkuu wa Apple, Bw. Tim Cook na kumuomba:
Apple iache kufanya biashara Urusi lakini ifunge kabisa upatikanaji wa Apple Store (kufunga App Store) lakini pia iache kufanya biashara nchini humo (Urusi).
Barua hiyo ambayo Naibu Waziri Mkuu ameichapisha kupitia mtandao wa Twitter alimalizia kwa kuwa na matumaini vikwazo hivyo vitashinikiza vijana wa Urusi kuomba nchi yake iachane na hicho ambacho inakifanya nchini Ukraine.
Apple waijatoa neno lolote kuhusiana na ombi la Ukraine lakini huko nyuma kampuni hiyo nguli kwenye masuala ya teknolojia ilisema inafanya kila linalowezekana kuhusu timu yake ya wafanyakazi walipo nchini humo na inaunga mkono huduma za misaada ya kijamii.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.