Licha ya Apple Watch Series 3 kuwa saa janja ya bei ya chini (punguzo) kutoka Apple kwa muda mrefu, saa hii yapigwa chini baada ya miaka mitano katika soko ili kupisha bidhaa hii >>
Kwa sasa Apple Watch hizi zitakua hazizalishwi kabisa na kampuni na hili linatokana na utambulisho wa saa mpya ambazo zimezalishwa na Apple.
Kilichotokea ni kwamba hakutakua na nafasi ya saa za series 3 kutoka kwao Apple, hili sio jambo la kushangaza sana kwani ni kawaida kwa kampuni kusitisha bidhaa fulani kama wakitoa nyingine.
Sababu mara nyingi huwa inakua ni kuipisha biashara/bidhaa mpya na yenyewe ipate uwezo wa kulitawala soko –kama itaweza—kwa muda.
Toleo la progamu endeshi jipya yaani WatchOS9 ndio toleo pekee ambalo halitakua likipatikana katika Apple Watch Series 3, hii ni moja ya sababu ya saa hiyo kulazimika kulipisha soko.
Ikumbukwe kuwa Series 3 iliotoka mwaka 2017 pamoja na iPhone X hivyo kuifanya kutumiza miaka mitano mpaka mwezi huu.
Kwa uwazi kabisa Series 3 ni saa ambayo ilileta mapinduzi makubwa sana katika soko zima la saa janja—kwa kifupi ni kwamba imefnaya kazi yake!
Niandikie hapo chini katika eneo la comment, je hii umeipokeaje? Unaona ni sawa kwa kampuni kama Apple kuachana na baadhi ya bidhaa zake za zamani?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.