Apple wamefunga maduka yake mengi yanayotambulika kama Apple Store katika miji mbalimbali ya nchini Marekani ili kuepeuka wizi zaidi.
Kwa siku kadhaa sasa kuna maandamano makubwa yanaendelea katika miji mbalimbali nchini humo kupinga ubaguzi wa rangi. Maandamano haya yameendana na uvunjifu wa sheria unaohusisha ubomoaji wa maduka na wizi.
Hadi sasa tayari maduka ya Apple katika miji kadhaa – Portland, Philadephia, Brooklyn, Salt Lake City, Los Angeles, Charleston, Washington, Scottsdale na San Francisco yamekwishavamiwa na mali mbalimbali hasa hasa simu na laptop zikiibiwa.
Katika kuchukua hatua za kulinda wameamua kuanza kuyaziba maduka hayo.
Maandamano yanayoendelea nchini humo nje ya kuleta hasara kubwa kwa biashara mbalimbali – hasa hasa kipindi ambacho kuna janga la Corona lakini pia yamesababisha kuahirishwa kwa baadhi ya matukio. Sony wameahirisha utambulisho rasmi wa PlayStation 5 na pia Google wameahirisha utambulisho wa Android 11, toleo jipya la Android.