Apple na Samsung wamekua wakichuana vikali sana katika soko la kutengeneza na kuuza simu. Ni sawa iko wazi wengi wetu tunapenda samsung, lakini kwa mwaka 2020 inabidi Apple ipewe heshima yake.
Ilikua imezoeleka sana kwa kampuni ya Apple kutoa simu moja kila mwaka mwezi wa tisa mara nyingi. Kwa mwaka huu wametoa simu mbili katika nyakati tofauti tofauti kabisa.
Kumbuka mwezi wa nne walitoa iPhone SE(2020) na mwezi wa kumi wakatoa simu ne yaani iPhone 12, iPhone 12 Mini, iPhone 12 Pro na iPhone 12 Pro Max.
Kwa mara ya kwanza ndio Apple wameweka utofauti katika simu zake za kawadia (iPhone 12 Pro) na zile kubwa zake (iPhone 12 Pro max) ambapo zamani simu zilikua zinatofautiana ukubwa tuu lakini sifa zake zilikua zinafanana tuu
Pengine huu ndio mwaka ambao kampuni imezindua na kutangaza vifaa vingi zaidi kuliko miaka yake mingine yote kwa harakaharaka mwaka huu wameachia simu tano, iPad Pro, Airpods, Airpods Pro (ambazo zinafunika kichwa), OS 14 (Mpya) n.k
Ukiachana na hayo yote bado vyanzo mbalimbali vya habari za kiteknolojia vimetoa orodha ya simu janja nzuri zaidi kwa mwaka 2020, iPhone 12 inashikilia namba moja ukilinganisha na simu zingine.
Ukiachana na vitu ambavyo Apple imefanya kwa mwaka 2020 hii haimaanishi kuwa Samsung hawajafanya lolote… unakumbuka zile simu tatu S20, S20+ and S20 Ultra zote zilitoka mwaka huu na zimefanya vizuri sana.
No Comment! Be the first one.