Taarifa zilizotoka ni kwamba Apple wanawekeza majeshi yao katika kampuni ya LG ili kuhakikisha kuwa wanatengeneza simu ambazo zitakua ni vioo vya kukunjika.
Kumbuka katika iPhone X, Apple inategemea vioo vya OLED kutoka kwa Samsung ambae pia ni msambazaji pekee wa vioo hivyo kwa Apple.
Teknolojia hii itaanza kufanyiwa kazi mara tuu ifikapo 2019 kwa sababu ndipo uzalishaji mkuu utakapoanza. Apple wanafanya kila njia ili na LG wawe wanawatengenezea vioo vya OLED na hii itasaidia kupunguza gharama za uzalishaji ukiangalia kwa sasa wanawategemea Samsung tuu ambao pia ndio washindani wao wa juu.
Kwa sasa kampuni ya Samsung ndio inaonekana kuwa na nafasi kubwa zaidi kuleta simu ya kujikunja mapema zaidi ya Apple.
Lakini unaweza ukashangaa teknolojia hii kwa Samsung inaweza ukaja mwakani tuu na wakaachia simu janja ambayo inakunjika katika kioo chake cha OLED. Kwa Apple ni mpaka 2020 ifike na unaweza shangaa kuwa simu zinaanza uzwa rasmi mwaka 2021.
Vile vile hapo mwanzoni zilitoka taarifa kuwa Apple ina mpango wa kutumia vioo kutoka Japan (Ambavyo vinapinda) katika simu zake zijazo.
LG wako mbioni kufungua kiwanda chao ambacho kitatumika katika kutengeneza vioo hvyo vya OLED na inasemekana kuwa Apple itachangia kiasi cha dola bilioni 2.6 kama sehemu ya uwekezaji.