Wengi tumezoea kuiona kampuni ya Apple ikiwa inajikita zaidi katika teknolojia ya simu na kompyuta, na kidogo suala la magari janja siku hizi…sasa imejiingiza katika sekta ya nishati.
Kampuni hiyo imetengeneza kiwanda kingine kinachojitegemea ambacho kitaweza kuzalisha umeme mwingi wa jua. Umeme huo utaisaidia kampuni katika ofisi zake na pia umeme unaobakia (unaozidi) wataweza wauzia watu wengine.
Kampuni mpaka sasa ina mashamba makubwa kabisa ya kufua umeme wa jua. Jina kamili la kampuni hiyo ya nishati ni Apple Energy LLC na inamilikiwa kwa 100% na Apple Inc.
Sio kitu cha achabu kuona kampuni ya Apple leo inakuja na nishati ya aina hii kwani tangia mwaka 2013 katika vituo vyake vyote vya data (data center) vilikua vinatumia umeme wa kufuliwa. Na mfano mzuri ni kwamba kampuni ina project yake yenye sola paneli zaidi ya maeneo 800 ambayo yanaendesha shughuli za kampuni huko Singapore.
Ukiachana na kutumia umeme waonaozalisha kupitia sola paneli zao, bado kampuni ina mpango wa kuyauzia makampuni mengine umeme unaosalia. Taarifa iliyopo ni kwamba kampuni itauza nishati hiyo kwa bei iliyopo sokoni muda huo.
Kampuni hiyo imeseama kuwa iko tayari na ina vigezo tosha vya kuuza umeme unaosalia kwa bei ile ile iliyopangwa sokoni kwa kuwa kampuni kama kampuni bado ni ngeni katika swala zima la kuuza umeme hivyo haitakuwa na nguvu ya kushawishi kupanda au kushuka kwa bei ya umeme katika soko.
Kama inavyofahamika kuwa awamu hii mauzo ya simu za Apple maarufu kama iPhone yemeshuka kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na vipindi vyote vya mauzo ya matoleo ya simu za aina nyingine. Pengine labda hii ni njia nyingine kwa kampuni kuweza kupapasa kona zingine ili kujihakikishia uhakika wa mapato.
Na pia kumbuka ni jambo zuri kutawanya biashara zako na kuwa na njia nyingi za kuweza kujipatia kipato.