Kwa miaka mingi tuu Apple kupitia bidhaa zao za Apple zimekuwa na vioo ya LCD ambavyo ni vizuri lakini havina teknolojia bora zaidi kuliko vile vya OLED ambavyo tutaanza kuviona kuanzia mwakani kwa Baadhi ya iPad.
Kwa wale ambao tunatumia au tumeshawahi kutumia iPad na inawezekana kabisa kutokana na ukuasji wa teknolojia hivi sasa unamiliki simu janja yenye kioo cha OLED basi ama kwa hakika unaijua tofauti kubwa ilivyopo kwenye vioo vya LCD na OLED.
Apple wanafikiria kuhamia kwenye vioo vya OLED kwa matoleo yajayo ya iPad kuanzia mwaka 2022. Ni mara chache sana kuona tabiti ikiwa na kioo cha OLED isipokwa Samsung Galaxy Tab S7 Plus, Lenovo Pad Pro, Galaxy Tab S6 na iPad Pro 2021. Ingawa Apple wameanza kutumia vioo vya OLED kwenye simu janja tangu mwaka 2017 lakini wameendelea kutumia LCD kwenye iPad.
Samsung, LG ndio wanaaminika kuwa wanahusika kutengeneza vioo hivyo vya OLED ambapo bidhaa hizo tutaanza kuziona kuanzia mwakani kwa baadhi ya iPad.
Kulikoni kwa Apple mpaka kuamua kutanua wigo wa vioo vya OLED kwenye iPad? Hatujui iPad hizo zitakuwa na sifa gani lakini kama una toleo la Pro 2021 utakuwa unajua utofauti wake na nyingine.
Tumeendeleza wimbi la kukuhabarisha basi na wewe usisite kutufuatilia kupitia mitandao yetu ya kijamii, tovuti kwa habari mbalimbali zinazohusu teknolojia.
Vyanzo: GSMArena, XDA Developers
One Comment