Google waleta na app itakayowasaidia watumiaji wa simu zake kuweza kuepukana na upigiwaji wa simu za usumbufu na matangazo kutoka huduma au watu wanaotaka kuwauzia bidhaa/huduma mbalimbali.
Simu hizo maarafu kwa jina la kimombo la ‘spam calls’, ni tatizo kubwa sana katika nchi zilizoendelea kuliko ata kwa nchi zinazoendelea. Google wanatengeneza toleo spesheli la app ya kupiga na kupokea simu kwa matoleo ya simu ya Android One, Nexus na Pixel.
Android One, ni mradi spesheli wa Google unaohusisha utengenezaji wa toleo jepesi la programu endeshaji ya Android na kuyapatia makampuni ya utengenezaji simu yenye nia ya kutengeneza simu za bei nafuu bila kuathiri utendaji kazi wa simu.
Nexus, ni familia ya simu za Android zinazobuniwa na kutengenezwa kwa ushirikano kati ya Google na makampuni mengine ya utengenezaji simu kama vile LG, Huawei, na wengine.
Pixel, ni familia mpya ya simu zinazotengenezwa na Google. Google wenyewe wameamua kuchukua nafasi kubwa katika ubunifu na kisha kusimamia utengenezaji wa simu za kiwango cha juu cha ubora zinazotumia Android.
Je, uwezo huu utafanyaje kazi?
- Namba ya simu ambayo imesharipotiwa na wengine wengi kama ni ya kutoka kwa huduma au mtu anayepiga simu za usumbufu akipiga simu;
- App ya kupiga na kupokea simu, ‘Phone’, itaigundua na moja kwa moja kuilazimisha iache ujumbe wa sauti – voicemail.
- Wewe kama mtumiaji simu hautapata notification/ujumbe wa kukuambia ya kwamba kuna simu imepigwa kwa wakati huo. Simu itakuwa kimya kama vile hakuna kilichotokea.
- Ila ukiingia kwenye app yako ya kupiga na kupokea simu ndio utaona ujio wa ‘missed call’ kutoka simu hiyo, pamoja na kukuonesha kama ujumbe wa sauti/voicemail uliachwa.
Google wanategemewa kutumia teknolojia ya akili-feki-ya-kompyuta (AI), kuweza kutambua namba za simu mbalimbali zinazochukuliwa kama SPAM. Tayari teknolojia yao katika kuchambua barua pepe hasa hasa kupitia huduma yao ya barua pepe ya Gmail inauwezo mkubwa wa kuzidi kusaidia kufanikisha kazi ya app hii.
Kwa sasa uwezo huo upo katika majaribio, ya kiwango cha BETA. Wengi wanategemea uwezo huo mpya utaanza kusambaa kwa watumiaji wengine wa simu za Android One, Nexus na Pixel.
Kama unatumia moja ya simu zenye sifa hii basi unaweza tembelea Google PlayStore hapa – Google PlayStore -> Download Google Phone
Usiogope kama hautimii simu hizo, tunaamini muda si mrefu Google kupitia toleo la Android wanaweza kuleta huduma hii kwa watumiaji wengi zaidi.