Neno Android lina maana kadhaa, ila kimsingi, yote yana maana nzuri na mwisho wa siku inaeleweka.
Neno Android linatumika sana kwenye intaneti, na inaweza kutumika kumaanisha kitu fulani wakati siyo chenyewe na bado mtu akaeleweka. Android inaweza kumaanisha mfumo wa vifaa vya kiganjani, simu, laptop, TV, na siku zinavyozidi kuenda, karibu kila kitu, hata roboti.
Katika kujaribu kulielezea neno ‘Android’, waandishi kama Jerry Hidenbrand wa AndroidCentral, wanaweza kumaanisha moja ya vitu vitatu:
‘The Open Android’ – Android Huria
Kampuni ya Google inaongoza utengenezaji wa programu-endeshaji huria (‘Open Source Operating System’) iitwayo Android. Programu-endeshaji hii ina kila kitu cha msingi na hata zaidi vinavyohitajika kuwasha na kutumia kifaa cha kielektroniki, na mtu au taasisi yoyote inaweza kuichukua na kuitumia itakavyo. Pamoja na mfumo huo kuna viwezeshaji pia vya kumpa urahisi mtu yoyote mwenye nia kutengeneza programu za ziada kwa urahisi, ambazo anataka zitumike kwenye kifaa chake.
Neno fasaha kwa Android hii ni The ‘Android Open Source Project’ (AOSP) na ndio kinachomaanishwa mtu anaposema Android ni huru na bure. Ina wezekana umeshawahi kucheza na Android kama hii kama umewahi ku-root na kuweka ROM yako kwenye kwenye simu yako. Watengenezaji wa ROM huchukua AOSP na kuirekebisha kufaa simu au tabiti aina flani.
Android inayotumiwa na Watu wengi

Kwa watu wengi, Android wanayoitumia siyo AOSP. Vitu kadhaa vinaweza kubadilishwa na kuongezwa kutengeneza Android tofauti kabisa.
Iwe una simu ya Nexus au ya Samsung au ya Motorola au simu nyingine yoyote inayoendeshwa na Android, kila moja inatumia Android iliyobadilshwa na kuongezewa mambo mambo flani tofauti.
Utofauti wa Android kama hii si wa bure na hauwezi kusambazwa kama unavyopenda kisheria ingawa watu hufanya hivi na hamna anayesumbuliwa. Utofauti unaokuja na Androidi hizi tofauti ndiyo unaoweka ushindani kwa watengenezaji tofauti wa Android. Watu wengine huchagua Samsung au HTC au Sony au nyinginezo kutokana na vitu kila moja ilivyonavyo.
Android Ulioshikilia Sasa

Kama wewe ni mtu unayefuatilia sana maswala ya Teknolojia na hasa teknokona, tayari unajua kwamba simu ulioshika ni ya aina gani – Samsung, Tecno, Sony, Huawei, yoyote. Hatahivyo, kuna watu, tena wengi ambao wao wanachojua ni kwamba wana simu ya ‘Android’.
Kama vile Lumia 535 ni Wndows Phone, Blackberry 8900 ni Blackberry na iPhone 4S ni iPhone, Tecno yako ni Android.
Kila Android ya kisasa inaweza kuendesha app zilezile, kutumia huduma za Google vilevile na hata kuunganisha watu kihisia sawia. Android tofauti zimetengenezwa kitofauti ila usawia unabaki palepale.
Kwahiyo, Android ni Nini Hasa?
Tumeeleza vitu vitatu vinavyoweza kumaanisha Android. Google wanatumia neno Android kumaanisha vitu viwili tofauti (na sisi watumiaji tunafanya hivyo) kwa sababu, mara nyingi inaeleweka wanachomaanisha!
Ukweli ni kwamba, ukimaansha Android kama AOSP, au kama simu yako ya Samsung au kama kuitofautisha simu yako na iPhone wakati wa mabishano ya ipi zaidi, Android ni Android – hata kama imewekewa manjonjo kadhaa kuifanya ionekana kidogo tofauti na Android nyingine.
Chukulia mjadala huu kama hivi:
1. Ukiona mfanyakazi wa Google akiandika kitu kama hiki mtandaoni:
“mkdir android ;
cd android ;
repo init -u git://android.git.kernel.org/platform/manifest.git ;
repo sync ;
make”
mtu huyu anamaanisha moja ya maana ya Android
2. Ukisikia au kuona kampuni ya Google au kampuni ya Sony, Samsung au HTC ikitangaza simu yao mpya ya Android, wanamaanisha Android nyingine: ya kwao!
3. Ukisikia rafiki yako kanunua simu mpya ya Android kutoka duka la simu, hiyo ni maana nyingine ya Android!
Picha Na:
memegenerator.net, Google Inc, news24