Ukizungumzia simu janja za Samsung ambazo mpaka sasa zimeshapokea masasisho ya kuhamia Android 11 ni nyingi kwa idadi ambapo rununu mbalimbali ambazo kampuni hiyo inatengeneza zimeshawezeshwa kama Galaxy A10s!
Samsung wameendelea na kupeleka vitu vizuri kwa simu janja zake na safasi hii ni zamu ya Galaxy A10s ambayo ilitoka mwaka 2019 ikiwa na Android 9 Pie na safari yake ikaendelea polepole mpaka sasa imefika kwenye Android 11.
Simu janja hii imekuwa ikipokea masasisho mbalimbali ya kiulinzi kila mara ambapo yamekuwa yakitolewa na wahusika. Mbali na hilo simu hii haijafika kwenye Android 11 kwa kufumba na kufumbua tuu bali mwezi Aprili 2020 ndio iliwezeshwa kuhamia kwenye Android 10.
Masasisho ya kuweza kuhamia kwenye Android yameanzia Malaysia na Vietnam kwa utambulisho maalum, A107FXXU8CUG1 sambamba na yale yanayohusisha usalama wa simu janja ambapo inaaminika kuwa huenda yatakuwa ni masasisho ya mwisho makubwa kwenda kwa simu husika.
Siku zote ni kitu kizuri simu janja kuwezeshwa kuhamia kwenye toleo jipya la programu endeshi lakini daima tukumbuke kuhakikisha kuwa simu inakuwa na chaji zaidi ya 50%, kifurushi cha intaneti ambacho kinazidi GB 1.4 bila kusahau uwepo wa nafasi kwenye memori angalau GB 1.5 na zaidi.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.