Unapoona pameandikwa “Ali….” unanza kufikiri kuwa kitu hicho kitakuwa chini ya tajiri na bilionea Bw. Jack Ma. Na wala sio uwongo AliPay inamilikwa na mtu yuleyule mwenye Ailibaba.
Katika dunia la leo iliyotawaliwa na teknolojia miamala mingi inafanyika kielektroniki kwa sababu usalama pamoja na sababu nyinginezo. Lakini je, AliPay ni nini?
AliPay ni mfumo wa kufanya malipo kwa njia ya kidijitali ambao unawezesha kufanya miamala duniani ingawa kwa sasa ni Wachina wanaoishi Uchina au mtu mwenye akaunti ya benki ndio anaruhususiwa kufungua akaunti AliPay.
Makubaliano kati ya UEFA na Alipay.
Yapo makubaliano ambayo ambayo yamefikiwa kwamba Alipay kuweza kuwa njia mojawapo ya watu kufanya malipo ili kuingia viwanjani kuangalia mechi za UEFA kwa timu za taifa kuanzia mwaka 2018-2026 bila kusahau mashindano ya Euro 2020/24.
Hii ikimaanisha kwamba katika kiwanja ambacho mechi ya UEFA kwa timu za taifa inachezwa kwa siku hiyo mtu ataweza kulipia tiketi yake kwa njia ya Alipay kupata fursa ya kuingia kiwanjani kuangalia soka.
Mpaka sasa AliPay ina wateja 700m huko Uchina wanaotumia mfumo huo wa malipo lakini suala zima la kampuni hiyo kuingia makubaliano na UEFA huenda namba ya watumiaji ikaongezeka mara dufu.
Vyanzo: Telegraph, Forbes