Serikali ya nchini Algeria imezuia mitandao ya kijamii katika jitihada za kuzuia wizi wa mitihani ya shule za sekondari nchini humo.
Wanafunzi wa sekondari nchini humo walirudia mitihani yao siku ya jumapili baada ya kufutwa kwa matokeo ya mtiani huu uliofanyika mwanzoni mwa mwezi wa sita kufuatia kuvuja kwa maswali katika mitandao.
Mitandao ya Facebook pamoja na Twitter ni miongoni mwa mitandao ambayo imefungiwa kwa muda huko nchini Algeria katika kile kinachosemwa kwamba ni kuzuia wimbi la uvujishaji wa mitahani hiyo katika mitandao hiyo.
Wanafunzi wa shule za sekondari walifanya mitihani yao ya kuingia chuo kikuu mwanzoni mwa mwezi wa sita mwaka huu, katika hali ya kustaajabisha maswali ya mitihani hii yalizagaa Facebook pamoja na Twitter jambo ambalo lilisabibisha mitihani hiyo ifutwe.
Uvujaji wa mitihani si jambo geni sana kwa maana hata hapa kwetu tayari umekwisha tokea mara kadhaa, lakini ukuaji wa teknolojia unazidi kubadilisha mtazamo wetu juu ya jambo hili kwa kuwa unaongeza wepesi.
China ni moja ya nchi ambazo wizi wa mitihani unafanyika kwa kiwango kikubwa cha teknolojia lakini pia India imekuwa na matukio ya kustaajabisha ya wizi wa mitiahani.
Soma zaidi: Wanafunzi wa nchini China wapo juu kutumia teknolojia katika kuibia mitihani.
Serikali ya Algeria imesema kwamba kuzuiwa kwa Facebook Twitter na mitandao ya 3G ni kwaajiri ya kuwalinda wanafunzi dhidi ya majibu na maswali ambayo yanachapishwa huko. Watu kadhaa baado wanashikiliwa na serikali baada ya kukamatwa kwa shutuma za kuvujisha mitihani hiyo katika intaneti mwezi huu mwanzoni.
One Comment
Comments are closed.