Fikiria kama akaunti moja ya whatsApp ikiweza kutumika kwa vifaa mpaka vinne? Ndio ndio hili tulitegemee hivi karibuni kwani mkurugenzi mkuu wa WhatsApp bwana Cathcart, ameliongelea hilo.
Licha ya hivyo hata mmiliki wa kampuni hiyo ya WhatsApp pamoja na ile ya Facebook bwana Mark Zuckerberg aliwaambia WABetaInfo kwamba watumiaji wa App hiyo wakae tayari kwa kipengele hiki.
Toleo hili kama kawaida litaanza kwanza kutolewa ka ‘developers’ ndani ya miezi ya karibuni na kisa baadae ndio toleo litakuwa linapatikana kwa kila mtu.
Licha ya akaunti kuwa imeunganika kwa vifaa vinne kampuni bado inahakikishia watumiaji wake kuwa kipengele chake cha ulinzi na usalama cha ‘end-to-end encryption’ bado kitakua kinafanya kazi kama kawaida.
“Ni changamoto kubwa sana kuweza kuunganisha jumbe za akaunti moja ya WhatsApp kupitia vifaa vinne, lakini tayari tumeshapata ufumbuzi na hili litafanyika hata kama kifaa kimoja kitakua kimekwisha chaji” — Zuckerberg alisema
Vilevile, hawakuishia hapo bali walisema pia watu wajiandae kwa kipengele kipya ambacho kitajulikana kama “view once” ambapo hapa mtu anaweza soma jumbe mara moja tuu na kisha jumbe au taarifa hiyo inafutika.
Kipengele kingine ni “disappearing mode” ambapo hapa ukipawasha basi jumbe zako zote zitaweza kutoweka kila baada zikisomwa.
Ukiachana na hayo yote bado WhatsApp haikuweka wazi kuwa ni lini vipengele hivi viwili vitatoka rasmi, lakini kuhusu kutumika kwa vifaa vinne ni miezi ya usoni tuu
No Comment! Be the first one.