Labda wenyewe wamejipanga vizuri….au labda wamefanya makosa na muda si mrefu uamuzi huu utawang’ata wenyewe. Katika hali ya kitofauti Airtel waondoa bando la GB 1 kwa siku na kufanya kifurushi cha MB 400/kwa Siku kuwa Tsh 1000.
Soma Pia – TCRA: Ubora wa huduma kwa mitandao ya simu Tanzania!
Ushindani ni mkubwa kwa muda huu kuliko kipindi kingine chochote katika mitandao ya simu. Kuja kwa Halotel, mtandao uliowekeza zaidi kwenye huduma ya intaneti ya kiwango cha 3G kumeleta ushindani mkubwa kwa mitandao mingine yote – Airtel, Tigo, Zantel.
Kwa muda huu kila mtandao unajaribu kuja na kitu cha kuwavutia zaidi wengine, na kwa kweli ni jambo la kushangaza kuona Airtel wanachukua uamuzi ambao unaweza kuwaathiri zaidi.
Kufikia mwezi wa nne mwaka huu tayari data kutoka TCRA zilikuwa zinaonesha nafasi ya pili kwa namba ya wateja iliyokuwa inashikiliwa kwa muda mrefu na Airtel tayari inaonekana kuchukuliwa na Tigo. Ukijumlisha ukuaji wa haraka wa Halotel na ukuaji mkubwa wa ushindani si muda mrefu tutasikia Airtel ipo katika matatizo.
Uamuzi kama huu unaonekana umekaa kimapato zaidi na hivyo inaweza ikawa inaashiria ya kwamba kama wakiweka bei za ushindani za sasa basi watakua wanapata hasara kiuendeshaji…na kama ni hivyo basi wapo kwenye hali mbaya kibiashara…
Airtel still on 3G decided to Price hike their daily 1GB bundle to the same amount as Vodacom and Tigo..who have 4G? ?????
— Ricky (@Rickyboshe) August 11, 2016
Kila siku nikijiunga 1GB ni 30GB kwa mwezi,sasa nani anataka vifurushi vyenu vya uwongo vya mwezi vya 12GB for 35k https://t.co/EPFJgmxpF8
— Mere (@Ms_Mollel) August 11, 2016
Halotel https://t.co/48CLYKJGgA
— D.A.M.A (@davismazula_) August 11, 2016
@airtel_tanzania mnazingua mmewaona @Haloteltz na @Tigo_TZ wako fresh bila tatizo
— Lee Wes (@am_Cali) August 11, 2016
NINI KITAFUATA?
Watanzania wengi wanatumia laini zaidi ya moja, na pia hawaogopi kujaribu mtandao mwengine mpya kwao. Kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii – Facebook, Twitter, WhatsApp na kuperuzi sana kwa siku basi uamuzi huu hakika utawafanya wahamie upande wa pili. NA HILI LITAWAUMIZA AIRTEL MUDA SI MREFU.
Soma Pia – TCRA: Ubora wa huduma kwa mitandao ya simu Tanzania!