Adidas ni moja kati ya kampuni inayojihusisha na vifaa vya michezo na yenye jina kubwa sana na ni moja kati ya makampuni makongwe katika nyanja hiyo.
Spika hizi za masikio inasemekana kuwa zitakaa na chaja ya kukuwezesha kusikiliza –nyimbo n.k- kwa masaa 80 au hata zaidi kama zitakua kwenye jua muda wote.
Kwa dunia ya leo ukisema vifaa ambavyo vinatumia nishati ya jua kwa maana ya sola inakua sio jambo la kushangaza sana kwani teknolojia hii kwa kiasi kikubwa imeshazoeleka.
Jina la spika hizi za masikio zisizokuwa na nyaya (wireless) linajulikana kama RPT-02 SOL na teknolojia ya sola inayofanikisha spika hizi kufanya kazi inaitwa Powerfoyle.
Teknolojia hiyo ndio ambayo inafanya mwanga wa kawaida na juu kubadilika na kuwa nishati ambayo inawasha spika hizo.
Pengine labda hatujazoea makampuni yenye mienendo sawa na kampuni kama Adidas kujikita katika kuleta bidhaa za namna hizi, lakini kumbuka teknolojia inakua kila siku.
Kingine ni kwamba sababu kampuni inajihusisha sana na vifaa vya michezo basi hata spika hizi za masikio na muhususi kabisa katika kufanyia mazoezi –kukimbia n.k.
Spika hizi kutoka katika kampuni ya Adidas zitaanza kuingia sokoni rasmi ifikapo tarehe 23 mwezi agosti mwaka 2022 na zitakuja na rangi mbili, kijivu na njano.
Ningependa kusikia kutoka kwako niandikie hapo chini katika eneo la comment, je hii umeipokeaje? Unatamani kutumia spika hizi za masikio?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.