ZTE wamekuja na simu inayobeba jina la ZTE Axon M, simu hii inayotumia programu endeshaji ya Android imekuja na display mbili.
Kwa haraka haraka kupitia ZTE Axon M, ZTE wanataka kufanikisha jambo ambalo wengi wameshakuwa wakijiuliza mara nyingi tuu – kwani ni lazima simu ya mkononi iendelee kuwa kama ilivyo ata baada ya miaka mingi tokea tuanze kuzitumia?
Ifahamu simu ya ZTE Axon M kwa undani;
- Inadisplay (vioo) viwili na hivyo unaweza kufunga na kufungua kama vile unachoweza kufanya kwa ‘wallet’ (pochi ya kiume).
- Display/Screen (Vioo) ni viwili vya ukubwa wa inchi 5.2 LCD kila moja. Display moja ipo kwenye uso wa simu na display nyingine ndio inayofunguka na kufungwa pembeni.
Simu hii inakuja na kamera ya megapixels 20, ukitaka kujipiga selfi inatumika hiyo hiyo kwani utaweza kujiona kupitia display nyingine.
Prosesa ya Qualcomm Snapdragon 821 na RAM ya GB 4,
Inakuja na toleo la Android Nougat ila tayari ZTE wamesema simu hiyo itapata sasisho la toleo la Android Oreo.